MWINGILIANOTANZU KATIKA UAINISHAJI WA TANZU ZA FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI.

Main Article Content

Jackline Murimi
Samwel Obuchi
Mark Kandagor

Abstract

Makala hii imejikita katika kujadili mwingilianotanzu katika uainishaji wa tanzu za fasihi
simulizi ya Kiswahili. Mwingilianotanzu hurejelea namna utanzu ulivyotagusana na tanzu
zingine na matini yote kwa ujumla ili kuboresha uwasilishaji wa ujumbe. Kama anavyosema
Mulokozi (1989), hakuna utanzu wowote ule uliojitosheleza ila tanzu huingiliana na matumizi ya
tanzu zingine ili kufaulisha uwasilishaji wa ujumbe. Mwingilianotanzu hutumiwa na mwandishi
kwa kujua au kwa kutojua. Dhana ya mwingilianotanzu inaondoa mipaka ya kazi husika na
kuiweka wazi kutazamwa kwa kuzingatia jinsi ilivyojumuisha mitindo na mbinu mbalimbali kwa
mfumo uliosukwa taratibu ili kuwasilisha ujumbe wake. Wamitila (2008) anadahili kuwa
mwingilianotanzu katika kazi moja hutoa nafasi kubwa ya msanii kujieleza barabara.

Downloads

Download data is not yet available.

Article Details

How to Cite
Murimi, J., Obuchi, S., & Kandagor, M. (2016). MWINGILIANOTANZU KATIKA UAINISHAJI WA TANZU ZA FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI. IJRDO- Journal of Educational Research, 1(2), 01-09. https://doi.org/10.53555/er.v1i2.488
Section
Articles